TAIFA STARS YAPATA KICHAPO KIKALI BOTSWANA

No Comments
taifa-stars-2014
Timu ya Taifa (Taifa Stars) imevurumishwa mabao 4-2 katika mechi ya kirafiki na Botswana jana.
Mechi hiyo iliyofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Gaborone ni sehemu ya maandalizi ya Taifa Stars kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika dhidi ya Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabao ya Taifa Stars yalifungwa na Khamis Mcha `Vialli` na nahodha wa Azam fc, John Raphael Bocco `Adebayor`
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajiwa kurejea nchini Julai 6 mwaka huu kuendelea na programu nyingine kwa ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji.
shaffihdauda.com

Dear readers, after reading the Content please ask for advice and to provide constructive feedback Please Write Relevant Comment with Polite Language.Your comments inspired me to continue blogging. Your opinion much more valuable to me. Thank you.