WORLD CUP: SHUHUDIA MABINGWA NA WALIOTWA ZAWADI ZA MASHINDANO MESSI, POGBA WAIBUKA KIDEDEA

WORLD CUP: SHUHUDIA MABINGWA NA WALIOTWA ZAWADI ZA MASHINDANO MESSI, POGBA WAIBUKA KIDEDEA

No Comments
Embedded image permalink
Embedded image permalink

Lionel Messi wins the Golden Ball.
Embedded image permalink
GOLDEN GLOVE – Manuel Neuer wins
Embedded image permalink
FAIR PLAY AWARD: Colombia

Embedded image permalink
POGBA MCHEZAJI BORA CHIPUKIZI
Embedded image permalink
GOLDEN BOOT: James Rodriguez
Embedded image permalinkEmbedded image permalink
Mario Gotze’s winner was the 32nd sub goal of the tournament,a record
HIVI NDIVYO ARGENTINA WALIVYOKUFA MBELA YA WAJERUMANI

HIVI NDIVYO ARGENTINA WALIVYOKUFA MBELA YA WAJERUMANI

No Comments
Mario Goetze of Germany scoresMario Goetze of Germany celebrates scoring his team's first goal in extra time as referee Nicola Rizzoli signalsMario Goetze of Germany celebrates scoringPhilipp Lahm of Germany reacts after a challenge by Rodrigo Palacio of Argentina Mario Goetze of Germany celebrates scoringMario Goetze of Germany celebrates scoringGeneral view during the 2014 FIFA World Cup Brazil Final match between Germany and Argentina Gonzalo Higuain of Argentina and Manuel Neuer of Germany

PSG YATAKA KUIPOKONYA TONGE MDOMOMI MAN UNITED, DI MARIA HUENDA AKATUA UFARANSA

No Comments
KLABU ya Paris Saint-Germain ipo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kumpata winga wa Real Madrid, Angel Di Maria, ambaye pia anatakiwa na Manchester United. 
Mshambuliaji huyo wa pembeni wa Argentina mustakabali wake haueleweki Bernabeu baada ya Real kuwa katika mpango wa kumsajili nyota wa Colombia, James Rodriguez. 
Pamoja na hayo, kocha Carlo Ancelotti hayuko tayari kumpoteza Di Maria, ambaye alikuwa na mchango mkubwa msimu uliopita wakati Real ikitwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, ingawa Rais Florentino Perez amemtambulisha Rodriguez kama 'galactic mpya'.
Yuko juu: Di Maria alikuwa ana msimu mzuri uliopita Real Madrid na sasa yuko njiani kuondoka

PSG sasa wanaamini wanaongoza mbio za kuwania saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, Di Maria, ambaye ana miaka minne katika Mkataba wake ya kuwa kazini Madrid. 
Real inaweza kusikiliza ofa ya kuanzia Pauni Milioni 50 kumuuza Di Maria owe kutoka kutoka PSG na United.

ROBBEN AMCHOMOLEA MACHO KWA MACHO VAN GAAL SUALA LA KUHAMIA MAN UNITED

No Comments
WINGA Arjen Robben amesema alimkatalia kocha wake wa timu ya taifa, Louis van Gaal wazo la kujiunga na klabu yake mlya, Manchester United.
Van Gaal ameipa Uholanzi nafasi ya tatu katika Kombe la Dunia baada ya jana kuifunga mabao 3-0 Brazil na baada ya hapo, Robben amesema kwamba kocha huyo mwenye umri wa miaka 62 alimtaka katika timu yake mpya, Old Trafford.
"Baada ya mechi aliniomba nije Manchester," Robben alisema akihojiwa na kituo cha Televisheni cha Uholanzi, NOS.
Amekosekana: Louis van Gaal amemkosa Arjen Robben aliyetaka kuhamia nays Manchester United

Lakini kwa bahati mbaya kwa mashabiki wa United, Robben amepiga chini ombi hilo na kusema: "Nina furaha sana kwa mahali nilipo. Nilimuambia (Van Gaal) hivyo. Van Gaal ni kocha bora niliyewahi kuwa naye. Tumekuwa a uhusiano mzuri sana, lakini siwezi kuhama. Niko sehemu sahihi Bayern, hivyo sina cha kufanya na Van Gaal au United,".
Baadaye na Van Gaal akathibitisha nia yake ya kumsajili Robben atue Old Trafford. "Wakati wowote anakaribishwa. Lakini anajua hiki yeye mwenyewe,"amesema.
Pals: Robben said he had a 'special' relationship with Van Gaal but rejected an Old Trafford switch
Twende Old Trafford: Van Gaal ameshindwa kumshawishi Robben ahamie Old Trafford
SHAMRA SHAMRA ZA MWISHO KOMBE LA DUNIA 2014

SHAMRA SHAMRA ZA MWISHO KOMBE LA DUNIA 2014

No Comments
The World Cup trophy sits on displayFormer Spanish international Carles Puyol and model Gisele Bundchen walk in the tunnel to present the World Cup in a Louis Vuitton travel caseSinger Ivete Sangalo and musician Carlinhos Brown perform during the closing ceremonyMusician Wyclef Jean and singer Alexandre Pires perform during the closing ceremonyMusicians Carlos Santana, Wyclef Jean, Shakira, her son Milan, Alexandre Pires are seen on stage during the closing ceremonyArtist perform during the closing ceremonyFIFA President Joseph S.Blatter attends with  Brazilian President Dilma Rousseff  and  Russian President Vladimir PutinFIFA Secretary General Jerome Valcke, Vanessa Lorenzo, NFL athlete Tom Brady, model Gisele Bundchen, and Carles Puyol look onArgentina fans enjoy the atmosphereGermany fans enjoy the atmosphere Former Brazilian international Kaka, former Brazilian international Pele and former England international David Beckham look onDancers perform during the closing ceremony
LUIZ FELIPE SCOLARI ANA `ROHO YA PAKA`, HII NDIO KAULI YAKE BAADA YA KUCHAPWA 3-0 NA UHOLANZI!!

LUIZ FELIPE SCOLARI ANA `ROHO YA PAKA`, HII NDIO KAULI YAKE BAADA YA KUCHAPWA 3-0 NA UHOLANZI!!

No Comments
434667_heroa
LUIZ Felipe Scolari amesema hatajiuzulu katika nafasi yake ya ukocha wa timu ya taifa ya Brazil, licha ya timu yake kufungwa mara ya pili mfululizo ndani ya siku tano.
Brazil walifungwa mabao 7-1 katika mechi ya nusu fainali iliyopigwa Belo Horizonte siku ya jumanne ya wiki hii na usiku wa jana walifungwa mabao 3-0 na Uholanzi na kumaliza katika nafasi ya nne ya fainali za 2014 za kombe la dunia kwenye ardhi yake.
Kabla ya mashindano haya, Brazil  ilikuwa haijapoteza mechi nyingi za nyumbanii tangu mwaka 2002 na walikuwa hawajawahi kufungwa nyumbani katika mashindo ya mpira wa miguu tangu mwaka 1975, lakini kufungwa mara mbili mfululizo ndani ya siku tano kumewachangaya mashabiki  na waandishi wa habari wan chi hiyo.
Lakini Scorali alikutana na waandishi wa habari baada ya kufungwa na Uholanzi na kusisitiza kuwa shirikisho la soka nchini Mbrazil litaamua hatima yake ya baadaye.
“Ulikuwa mchezo wenye nguvu sawa,” alisema. “Wachezaji wanatakiwa kupongezwa kwa jinsi walivyocheza. Hatukucheza vibaya-hayo ndio maoni yangu”.
“Kwasasa sio muda muafaka wa kuzungumzia hilo, “ alisema Scolari. “Nitaandika ripoti yangu na kumwambia rais wa CBF ni kitu gani nadhani hakikwenda sawa, yeye ataamua nini anataka kwa baadaye. Tumepoteza mechi nyingine, lakini maisha yanaendele”.
“Mwaka mmoja uliopita nilishinda kombe la mabara,” aliongeza. “Makosa hayako kwa makocha. Kitu ni kwamba tuna timu ya vijana sana. Hatujazalisha wachezaji wa kutosha, kwahiyo sio kazi rahisi hata kama Kocha mwinine atakuja”.
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3420#sthash.XHpGayew.dpuf

LOGARUSIC AELEZEA ANAVYOTAKA KUSHANGILIA USHINDI WA SIMBA

No Comments

Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema anataka kuwa na furaha na hakuna kitakachomfurahisha zaidi ya kuona kikosi chake kinashinda.

Loga raia wa Croatia amesema anataka kuwa na maandalizi ya uhakika katika kipindi cha sasa kwa kuwa ndiyo muhimu kumpatia ushindi.
“Ukikosea katika kipindi cha mwanzo, basi ujue una kazi ngumu. Furaha ya kufanya vizuri ni jambo jema kwa kocha yoyote.
“Natamani kushangilia kila wakati, lakini najua furaha itapatikana kama nitafanya mambo ya uhakika sasa na wachezaji wanapaswa kujituma na kunivumilia,” alisema Logarusic.
Tayari Loga ametua jijini Dar es Salaam na anaanza kazi kesho kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kujiandaa na msimu mpya wa 2014-15.

GEOFREY NYANGE KABURU KWA HILI SINA TATIZO NA WEWE SIMBA SC

No Comments
KABURU
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
MAKAMU wa Rais wa Simba sc, Geofrey Nyange `Kaburu` ni miongoni mwa watu wenye mtazamo sahihi katika soka la vijana nchini Tanzania.
Inawezekana ana mapungufu yake kama ilivyo kwa mtu yeyote, lakini mara zote mtazamo wake wa kuendeleza soka la vijana katika klabu ya Simba unanivutia sana.
Ili kutengeneza mfumo na falsafa ya klabu, huwezi kukwepa soka la vijana. Timu kama Barcelona zilianzisha mpira wa aina ya `Tiki -taka` . Huu ni mfumo wa kucheza mpira kwa kumiliki maeneo yote muhimu ya uwanja.
Mpira huu huwa wachezaji hawasimami eneo moja kama ilivyo kwa mifumo mingine. Wachezaji wanatakiwa kubadilishana nafasi kadri wawezavyo. Mlinda mlango pekee ndiye mchezaji anayebaki eneo moja.
Katika mfumo wa `Tiki-Taka`, beki anaweza kuwa mshambuliaji, kiungo anaweza kuwa beki, mshambuliaji anaweza kuwa beki ndani ya uwanja. Yaani kama beki wa kati amepanda, kiungo wa kati anarudi kukaba nafasi yake. Kama beki wa kulia amepanda kupandisha mashambulizi, winga wa kulia anaweza kushuka katika nafasi ya kulia kuzuia.
Ninachojaribu kusema ni kwamba kwenye mpira wa `Tiki-taka`, hakuna kukaa nafasi moja, yaani kama ni namba tisa unaweza kuwa mlinzi kwa muda wowote uwanjani au beki unaweza kushambulia .
IMG_1687Ramadhan Singano `Messi` (kulia) ni zao la Simba B
Huu ndio mpira waliocheza Barcelona kwa muda mrefu tangu wauasisi mwaka 1990, Mlanzi Johan Cruyff akiwemo. Walifanikiwa kuzisumbua timu nyingi za dunia hii. Haikuwa rahisi kuifunga Barca, na kwakuwa wachezaji wengi wa Barcelona walikuwa wanacheza timu ya taifa, wakajikuta wanahamishiwa mfumo huo kwa soka zima la Hispania.
Siku za karibuni, `Tiki-taka football` imekumbana na changamoto. Watu wamejua namba ya kucheza na mfumo huu. Hii inawalazimu Barca na Hispania kukaa chini kuboresha zaidi mpira huu na kuleta mpango B kwasabau huu unaelekeka kushindwa. Si kwamba mpira huu umekwisha, lakini wanatakiwa kuufanyia maboresho.
Ili ufanikiwe kucheza `Tiki-taka football`, moja ya vitu vya kuzingatia ni kuwa na wachezaji ambao wanaweza kucheza nafasi tofauti tofauti uwanjani.
Kwa maana ya mchezaji awe na uwezo wa kusimama nafasi tofauti, ili pale anapotakiwa kuwa beki anatakiwa kufanya hivyo. Na ili kuwapata wachezaji wa aina hii, lazima uwe na akademi za vijana wenye umri tofauti.
Barcelona wana akademi za vijana wa kila aina, wapo 6-10, 10-12, 12-14, 14-16, 16-17, 17-18, na kadhalika. Kwa mfumo huu ni rahisi kumuendeleza mchezaji na kumfundisha nafasi tofauti tofauti uwanjani.
Tiki-taka ni mfumo unaohitaji muda mrefu sana kufikia malengo.
Mkude5Jonas Mkude ni tunda la Simba B
Kaburu wa Simba wakati akiwa makamu mwenyekiti wa klabu hiyo enzi za utawala wa Ismail Aden Rage, alifanya kazi kubwa kuhakikisha Simba ya vijana maarufu kama Simba B inakuwa na mafanikio.
Kocha msaidizi wa Simba, Suleiman Abdallah Matola `Veron`, na aliyekuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya Simba, Ibrahim Masoud `Maestro` wakisaidiana na Kaburu walifanikiwa kuzalisha vijana wazuri.
Ramadhan Singano `Messi`, Said Ndemla, Jonas Mkude, Harun Chanongo, Edward Christopher, Wiliam Lucian `Gallas` ni moja ya matunda ya mpango huu makini.
Simba na Azam zimekuwa klabu za mfano kwa soka la vijana. Wengine wanajikongoja, lakini kwa klabu hizi mbili angalau zina mwelekeo ingawa kuna changamoto.
Siku chache zilizopita, Kaburu alisimamia usajili wa wachezaji wawili vijana chini ya miaka 20, Peter Manyika Junior pamoja na beki kinda wa Mwadui ya Shinyanga, Ibrahim Hajibu Migomba.
Baada ya usajili huo, Kaburu alisema malengo ni kuijengga Simba B.
Kwa hili nampongeza Kaburu na wenzake, lakini nadhani imefika wakati wa Simba kuwa na mfumo rasmi wa kupata wachezaji wake.
Kama wanataka kuifanya Simba kuwa klabu bora, lazima viongozi wajikunje kujenga akademi  ya soka la vijana. Lengo liwe ni kuchukua vijana wa umri mdogo zaidi na kukuzwa katika mfumo na utamaduni wa Simba.
Hii itaifanya kuwa klabu ya kisasa. Kwanza wachezaji watakaozalishwa watakuwa wazalendo kwa Simba. Kama mchezaji amekulia katika mazingira ya Simba, lazima aipende klabu yake.
Harun Chanongo (kulia) akiwakimbizi mabeki wa FC Libolo ya Angola kwenye moja ya mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika. Nyota huyo ni zao la Simba B
Uliona Fabregas, alikuwa Asernal, lakini bado akili ilikuwa Barcelona. Leo hii huwezi kumuondoa, Lionel Messi,  Iniesta, Harnandez katika klabu ya Barcelona. Wamekaa kwa muda mrefu na wanaona utumwa kutoka Katalunya.
Ili kuiga hili,  Kaburu lazima awekeze muda na fedha katika soka la vijana. Inaweza kuwa ngumu kutokana na uwezo wa klabu, lakini naamini Simba ina uwezo wa kufanya hivyo kama nia itakuwepo.
Amini usiamini, mpango huu wa soka la vijana utaibadilisha Simba. Kama Messi, Mkude, Chanongo ni muhimu kwasasa katika timu, basi mafaniko haya yanatakiwa kuwasukumu zaidi kuendeleza soka la vijana.
Kuna haja ya kutafuta utamaduni wa mpira wa Simba ili kuwajenga wachezaji katika mfumo mmoja. Na ili kufanikiwa, lazima pia waamue kuwaamini makocha na kuwapa muda zaidi.
Tafuteni walimu wanaoendana na mpira mtakaobuni katika klabu ya Simba  ili wafanye kazi na vijana wenu kutengeneza mpira rasmi wa Simba.
Leo Milovan, kesho Liewig, keshokutwa kibadeni, mtondo Logarusic. Hapa mtakuwa mnajidanganya tu.
Kaburu kwa hili sina tatizo nawewe, nitakuunga mkono kwa ushauri pia.
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3434#sthash.sdMUKkXB.dpuf
TAIFA STARS YAPATA KICHAPO KIKALI BOTSWANA

TAIFA STARS YAPATA KICHAPO KIKALI BOTSWANA

No Comments
taifa-stars-2014
Timu ya Taifa (Taifa Stars) imevurumishwa mabao 4-2 katika mechi ya kirafiki na Botswana jana.
Mechi hiyo iliyofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Gaborone ni sehemu ya maandalizi ya Taifa Stars kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika dhidi ya Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabao ya Taifa Stars yalifungwa na Khamis Mcha `Vialli` na nahodha wa Azam fc, John Raphael Bocco `Adebayor`
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajiwa kurejea nchini Julai 6 mwaka huu kuendelea na programu nyingine kwa ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji.
shaffihdauda.com
MZEE WA KUNG'ATANG'ATA LUIS SUAREZ HUYOO BARCELONA

MZEE WA KUNG'ATANG'ATA LUIS SUAREZ HUYOO BARCELONA

No Comments
article-2677164-1F43D0D600000578-630_634x347
Anaondoka? Liverpool na Barcelona wanatarajia kuanza mazungumzo juu ya kuuziana Luis Suarez.
KLABU za Liverpool na Barcelona zinatarajia kuanza kufanya mazungumzo juu ya bei ya awali ya paundi milioni 80 ili kuuziana mshambuliaji mweye matatizo kwa sasa, Muurguay, Luis Suarez.
Mtandao wa michezo wa Sportsmail unafahamu kuwa maofisa wa Liverpool, akiwemo mkurugenzi mtendaji, Ian Ayre, wamekubali kukutana na mkurugenzi wa michezo wa FC Barcelona, Raul Sanllehi,  mjini London ili kujadiliana thamani ya mchezaji huyo mwenye miaka 27.
Barcelona wanatazamiwa kutoa paundi milioni 60 kwa kuzingatia kuwa Suarez amefungiwa miezi minne kucheza soka baada ya kumng`ata beki wa Italia, Giorgio Chiellini.
Liverpool hawapo tayari kushusha bei ya Suarez, lakini wanataka kumhusisha mshambuliaji wa Barcelona Alexis Sanchez kama sehemu ya makubaliano hayo.
Controversial: Suarez has been linked with a move to Barcelona after being banned from football for four months
Suarez anahusishwa kujiunga na Barcelona baada ya kufungiwa miezi minne kucheza soka.
Barcelona wanasema mchezaji wao wa kimataifa wa Chile ana thamani ya paundi milioni 35, lakini tayari wameshakataa ofa ya paundi milioni 20 kutoka kwa Juventus ya Italia iliyokuwa na nia ya kumsajili nyota huyo mwenye miaka 25.
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=2969#sthash.oxTLgBpp.dpuf
HABARI MBAYA KWA WAFARANSA KOMBE LA DUNIA

HABARI MBAYA KWA WAFARANSA KOMBE LA DUNIA

No Comments
Ribery nje ya Kombe la Dunia
Mkufunzi wa Ufaransa amedhibitisha kuwa mshambulizi Frank Ribery hatashiriki kombe la dunia kutokana na jeraha.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 na anayechezea klabu ya Bayern Munich alijeruhiwa mgongoni wakati wa mazoezi siku ya Ijumaa.

‘’Hataweza kufanya mazoezi wala kucheza kwa majuma kadhaa.”“Ilimbidi kuwacha kufanya mazoezi kwa kuwa alikuwa akihisi uchungu mwingi sana,” Deschamps aliwaambia wanahabari baadaye.

Ribery amejeruhi mgongo mazoezini
Lyon's Clement Grenier pia atakosa mashindano hayo kwa jeraha la nyonga.
Kiungo cha kati wa Southampton Morgan Schneiderlin na mshambulizi wa Montpellier Remy Cabella wamejumuishwa kikosini ili kucheza kwa niaba ya wawili hao.
Ribery alipelekwa kupigwa picha ya MRI, ambayo ilidhibitisha kiwango cha jeraha hilo.

Riberi alichaguliwa kuwa mchezaji wa tatu bora zaidi duniani mwaka wa 2013 nyuma ya mshindi wa Ballon d’Or Christiano Ronaldo wa Real Madrid na mshambulizi wa Barcelona Lionel Messi.
SAKATA LA WAMBURA SIMBA LAIBUKIA FIFA

SAKATA LA WAMBURA SIMBA LAIBUKIA FIFA

No Comments
20131102-114737.jpg

Wanachama Simba waenda FIFA….

By Israel Saria on June 5, 2014
Wasema Malinzi anambeba Wambura!
WANACHAMA watano wa Simba wametuma barua katika Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wakimshtaki, Rais wa Shirikisho la Mchezo huo Nchini (TFF), Jamal Malinzi, wakidai ‘anampendelea’ aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Rais katika Uchaguzi Mkuu wa Simba, Michael Wambura.
Kamati ya Uchaguzi ya Simba ilimuengua Wambura katika mchakato wa uchaguzi kutokana na mgombea huyo kusimamishwa uanachama tangu Mei 5 mwaka 2010 kufuatia kufungua kesi kwenye Mahakama ya Kisutu yenye namba 100/2010 akiushitaki uongozi uliokuwa madarakani wakati huo.
Wanachama hao watano wa Simba waliowasilisha malalamiko yao FIFA dhidi ya Malinzi ni pamoja na  Masoud Hassan mwenye kadi namba 0500, Salehe Shahame (05596), Frank Pastoli (01288), Rajab Mtitu (01146) na Ally Mkumba (02519).
“Wambura ana kesi ya kimaadili na Kamati za Uchaguzi hazina mamlaka ya kuziamua kwa sababu kupeleka masuala ya soka kwenye mahakama za kawaida ni kosa kama katiba ya FIFA inavyoeleza,” ilisema sehemu ya barua hiyo.
Wanachama hao wa wadai katika barua hiyo iliyoandikwa Juni 3 mwaka huu kuwa Malinzi anadaiwa kuishinikiza Kamati ya Rufaa na Kamati ya Maadili kumrejesha Wambura kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi licha ya kufanya kosa hilo linaloenda kinyume na katiba ya Simba, TFF na FIFA.
Katika barua yao wameeleza kwamba tayari Malinzi ameshatoa maelekezo kwa kamati ya Rufaa imrejeshe mgombea huyo kwenye uchaguzi huo.
Katika barua hiyo wanachama hao wametuma nakala kwa viongozi wanaoshughulika na masuala ya uanachama ambao ni Thiery Reganass, Primo Corvaro na Ashford Mamelodi.
Malinzi aliliambia gazeti hili jana kwamba yeye na TFF haina nia ya kuingilia mchakato wa uchaguzi wa Simba ambao unatarajia kufanyika Juni 29 mwaka huu.
Kiongozi huyo wa juu alisema kwamba shirikisho hilo inachofanya ni kuhakikisha katiba na kanuni za uchaguzi kwa wanachama wake zinafuatwa.
Tayari kamati ya Rufaa ya Uchaguzi imesema kuwa itasikiliza rufaa ya Wambura Jumatatu Juni 9.
TANZANIASPORT
MBEYA CITY MWENDO MDONDO YALAMBA MKATABA WA MILIONI 360

MBEYA CITY MWENDO MDONDO YALAMBA MKATABA WA MILIONI 360

No Comments
Kampuni ya Bin Slum Tyre Company Limited leo imeingia mkataba rasmi wa kuidhamini timu ya soka ya Mbeya City Council ya jijini Mbeya katika hafla fupi ya utiaji saini mkataba huo iliyofanyika katika ukumbi wa ofisi za jiji la Mbeya, Mkataba huu utakuwa wa miaka miwili, ambao utawafanya Mbeya City kunufaika na kiasi hicho cha fedha kwa muda huo wote wa mkataba.
Binslum 2Binslum 8Mkataba huo wenye thamani ya milioni 360 ambao kampuni hiyo itakuwa ikitangaza bidhaa za RB Battery katika jezi za timu ya Mbeya city, na pia chini ya namba nyuma ya jezi itaandikwa kampuni ya Bin Slum Tyre Company.
Binslum 4Akiongea wakati wa utiaji saini wa mkataba huo jijini Mbeya, Mkurugenzi wa , Binslum Tyre Mohamed Binslum, alisema “Tumefikia makubaliano haya baada ya kuona uongozi wa timu ya Mbeya City umejipanga vizuri katika kuendesha timu yao, na kupata mwitikio mkubwa kutoka kwa wananchi wa Jiji la Mbeya pamoja na mikoa ya Kanda ya Kusini, hivyo itakuwa ni fursa nzuri kwa kuzitangaza betri zetu za RB ambazo pia Mbeya ni soko letu kubwa”.” Kampuni yetu ina bidhaa nyingi kama vile aina nzuri ya matairi ya Double Star na Vee Rubber”. Aliongeza Binslum.
IMG_20140605_120725Meya wa jiji la Mbeya Mheshimiwa Athanas Kapunga, ameishukuru kampuni ya Binslum kwa kukubali kuingia mkataba huo ambao utaisaidia timu kuongeza ufanisi wa kuindesha timu yao. “Napenda kuishukuru mkurugenzi wa Binslum Tyre Company Limited kupitia betri za RB kwa kuonyesha nia ya dhati katika kuedeleza soka la jiji la Mbeya na Tanzaniam kwa ujumla, nina imani msimu ujao tutakuwa na uwezo na kasi kubwa sana kama vile taa za gari zinavyotoa mwanga wa taa mkali zikiwa na betri za RB”. Alisema Meya wa jiji la Mbeya.
IMG_20140605_122200Naye Meneja masoko na uhusioano wa jamii wa kampuni ya Binslum Tyre Bw. Peter Ngassa alisema “Binslum Tyre Company tumeamua kuwekeza katika mpira wa miguu Tanzania kwa sababu kuna nafasi nzuri ya kutangaza bidhaa zetu kupitia eneo hilo na kutoa matokeo chanya pia kwa Mbeya City kutimiza ndoto zao”. Pia kupitia betri imara za RB tunaitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anaoutoa kila mara akiagiza makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini michezo kwa njia mbalimbali.
SHAFFIHDAUDA

STARS KUWASILI LEO, PONGEZI ZAMIMINIKA

No Comments

Kikosi cha Taifa Stars ambacho jana (Juni 1 mwaka huu) kiliitupa Zimbabwe (Mighty Warriors) nje ya michuano ya Afrika baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 kinarejea nchini leo (Juni 2 mwaka huu) kutoka Harare.


Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam saa 12.30 jioni kwa ndege ya Kenya Airways ikitokea Harare kupitia Nairobi.

Stars imefuzu kucheza raundi inayofuata kwa ushindi wa jumla ya mabao 3-2, kwani awali (Mei 18 mwaka huu) iliifunga Zimbabwe bao 1-0 katika mechi ya kwanza iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika raundi ya pili, Taifa Stars itacheza na Msumbiji ambapo itaanzia nyumbani kati ya Julai 19 na 20 mwaka huu, wakati mechi ya marudiano itafanyika Msumbiji kati ya Agosti 2 na 3 mwaka huu.

Wakati huo huo, Taifa Stars imeendelea kupokea salamu za pongezi kutoka kwa wadau mbalimbali baada ya kufanikiwa kuvuka kikwazo hicho cha kwanza katika harakati zake za kucheza Fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Salamu hizo zimetoka kwa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Manyara (MARFA), mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) akiwakilisha Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA), John Kadutu, na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ahmed Idd Mgoyi.
SALEHJEMBE
BAADA KUTEMWA MAN U MOYES SASA AFUNGUKA

BAADA KUTEMWA MAN U MOYES SASA AFUNGUKA

No Comments
20140601-205709-75429461.jpg

Moyes: Laiti ningepewa muda Man United

By Israel Saria on June 1, 2014
*Asema kuna ofa nyingi lakini anapumzika
Kocha wa zamani wa Manchester United, David Moyes anaamini alistahili kupewa muda zaidi kuwanoa Mashetani Wekundu hao.
Moyes (51) aliyefukuzwa kazi akiwa mwezi wa 10 katika mkataba wake wa miaka mitano, anasema Man U haiwezi kurekebishwa haraka, bali inahitaji muda.
Anasema ni bahati mbaya kwamba hakupewa muda huo, kwamba amejifunza mengi katika muda huo na kwamba aliyemsaidia tu ni Mskochi mwenzake, Sir Alex Ferguson aliyempendekeza kuvaa viatu vyake baada ya kukaa hapo kwa miaka 26.
Moyes anasema amepata ofa nzuri kutoka kwa klabu moja au zaidi lakini anafikiria kupumzika nje ya soka kwa muda badala ya kuzikubali.
Inaelezwa kwamba Celtic, mabingwa wa Scotland wameshamfuata kutaka azibe pengo la Mskochi mwenzake, Neil Lennon.
“Naamini nitakuwa na busara zaidi na kocha mwenye ujuzi zaidi baada ya kuwa kocha pale Old Trafford,” anasema Moyes ambaye nafasi yake inachukuliwa na Mdachi Lous van Gaal.
Moyes anasema kwamba angepewa muda angetekeleza vyema mpango wake wa muda mrefu wa kuifufua United na kwamba baada ya kuondoka alitumiwa ujumbe wa kumtakia heri na wachezaji, wakiwamo Wayne Rooney na Darren Fletcher.
Anasema Fergie alimshauri baadhi ya maeneo ya kurekebisha na kufanyia mabadiliko, mipango aliyokuwa ameshaianza lakini cha kushangaza akafukuzwa kabla hata mchakato haujafika mbali.
Kinachoshangaza katika wakati wake huo wa miezi 10 ni Man U kuvunja rekodi kwa kufanya vibaya wakati ni kikosi kile kile kilichokuwa kimetwaa ubingwa msimu uliotangulia chini ya Fergie.
TANZANIASPORT.COM

FOOTBALL

ATHLETIC