BAADA YA KUTEMWA SIMBA WAMBURA KUKATA RUFAA

No Comments
WAMBURA


Mgombea wa urais katika klabu ya Simba aliyeondolewa kugombea na kamati ya uchaguzi ya klabu hiyo, atakata rufaa.
Michael Richard Wambura ameondolewa kushiriki uchaguzi kwa kuwa si mwanachama.

Kwa mujibu wa kamati hiyo, Wambura alisimamishwa uanachama kutokana na kitendo chake cha kuipeleka Simba mahakamani, lakini hakuwahi kurudishwa.

Lakini Meneja wa kampeni wa Wambura, Majaliwa Mbasa amesema watakata rufaa.

“Tutakata rufaa TFF kupitia kamati ya rufaa na tunaamini Wambura atapata haki yake agombee.
“Sisi tunaona si sawasawa kabisa, hivyo hatuwezi kuacha hili suala lipite tu,” alisema Mbasa.

Dear readers, after reading the Content please ask for advice and to provide constructive feedback Please Write Relevant Comment with Polite Language.Your comments inspired me to continue blogging. Your opinion much more valuable to me. Thank you.