MICHUANO YA CECAFA YAINGIA ROBO FAINALI

No Comments
Baadhi ya timu zitakazomenyana ni pamoja na Leopards ya Kenya, Al Merreikh na Al Sandy ambazo zinaongoza makundi yao
Mashindano ya kandanda ya kombe la Cecafa Nile Basin yanaingia robo-fainali Ijumaa na Jumamosi nchini Sudan huku timu mbili za Sudan, Al Merreikh na Al Shandy, na AFC Leopards ya Kenya zikiongoza makundi yao.
Al Merreikh na Victoria ya Uganda zilimaliza mechi zao za makundi na pointi saba kila mmoja lakini Merreikh ikaongoza kundi A kwa sababu ya wingi wa mabao.
Merreikh sasa itakutana na Academie ya Tchite Burundi ambayo Jumatano ilimeza bao 1-0 dhidi ya AFC Leopards ya Kenya, mfungaji akiwa ni Bernard Mangoli.
Victoria inapepetana na Mbeya City, Leopards dhidi ya Defence ya Ethiopia, Al Shandy inakwaruzana na jirani wao wa Sudan Kusini, Malakia.
Katika mechi za Jumatano, Leopards ilishangiliwa sana na baadhi ya wanafunzi wa Kenya wanaosomea Sudan pamoja na balozi wa Kenya nchini humo Abrown Suge na naibu wake Maurice Nakitare.
Leopards itakua bila wachezaji wake mhimu Allan Wanga, Jacob Keli, James Situma na Wycliffe Kasaya ambao wako na timu ya taifa Harambee Stars kwa mechi yao na Comoros Ijumaa ya kufuzu kwa fainali ya mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika.
Etincelles imerudi nyumbani bila ushindi, na hawatasahu mechi yao ya mwisho dhidi ya Mbeya City waliposhindwa kufunga penalti, huku Al Shandy ikiicharaza Defence mabao 2-0, wafungaji wakiwa ni Nadir Eltyab na Omar Mahmoud.
BBC

Dear readers, after reading the Content please ask for advice and to provide constructive feedback Please Write Relevant Comment with Polite Language.Your comments inspired me to continue blogging. Your opinion much more valuable to me. Thank you.