REAL MADRID YAADHIBIWA KWA UBAGUZI WA RANGI

No Comments

Shirika la kandanda la Europa, UEFA, limeiwekea vikwazo timu ya mpira ya Real Madrid kwa makosa ya mashabiki wao, waliotoa ishara na kejeli za ubaguzi wa rangi wakati wa moja ya mechi zake.

Tukio hilo lilifanyika April wakati wa mechi ya nusu fainali kati ya mabingwa hao wa sasa wa kombe hilo la UEFA, na mahasimu wao,mabingwa wa zamani wa Bayern Munich.

Miongoni na adhabu walizopewa ni kufunga maeneo mawili ya uwanja wao wa Bernabeu wakati wa mechi yao itakayokuja ya UEFA na watapaswa kuweka mabango yaliyo na maandishi 'No to Racism' yaani 'Twakataa ubaguzi wa rangi!.

Dear readers, after reading the Content please ask for advice and to provide constructive feedback Please Write Relevant Comment with Polite Language.Your comments inspired me to continue blogging. Your opinion much more valuable to me. Thank you.