MBWANA SAMATTA MWIBA TP MAZEMBE

No Comments
TP Mazembe 1-0 AS Vital
TP Mazembe walishindi mahasidi wao wa jadi AS Vita kutoka Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo katika mechi iliyobashiriwa kuwa ngumu ya kundi A ya kuwania ubingwa wa Afrika miongoni mwa vilabu .
Mechi hiyo ya Jumapili ilichezwa katika hali ya taharuki kufuatia matukio yaliyopelekea kufa kwa mashabiki 15 katika uwanja wa Tata Raphael ulioko Kinshasa yapata majuma mawili yaliyopita timu hizo zilipokutana katika mechi ya ligi ya nyumbani.

TP Mazembe walishinda mechi hiyo kwa bao 1-0.

Bao la pekee la mechi hiyo lilifungwa na Aly Samata katika dakika ya 62 na kuihakikishia Mazembe ushindi kwa mara ya pili dhidi ya mahasimu wao hao.
Kufikia sasa timu zote zilizo katika kundi A zimeshinda mechi moja moja baada ya klabu ya Misri, Zamalek, kuishinda Al Hilal ya Sudan jijini Kairo na kunyakua pointi 3.

Ahly iliilaza Esperance ingawa walipoteza kwa kutocheza mechi yao ya nyumbani kufuatia machafuko ya wafanyikazi katika mji upatikanao katika pwani ya Tunisia, Sfax.

Dear readers, after reading the Content please ask for advice and to provide constructive feedback Please Write Relevant Comment with Polite Language.Your comments inspired me to continue blogging. Your opinion much more valuable to me. Thank you.