BRAZIL FUNGA KAZI: VIKOSI 150,000 KULINDA KOMBE LA DUNIA

No Comments
brazuka
Mawaziri wa ulinzi nchini Brazil wameweka wazi kuwa zaidi ya vikosi vya kijeshi laki moja na nusu (150,000) vitasambazwa nchini humo kuhakikisha kunakuwa na usalama wa kutosha wakati mashindano ya mwaka huu ya kombe la dunia.
Kwa mara ya kwanza mpira unarejea katika ardhi yake ya nyumbani kwa zaidi ya miaka 60 wakati Brazil ikiwa katika maandalizi ya mwisho ya kuwa mwenyeji wa michuano hiyo mikubwa zaidi duniani ambapo kwa kiasi fulani hali ya usalama imeonekana kuwa si nzuri kufuatia maandamano ya hapa na pale.
brazuka2
Kumekuwa na maandamano ya wananchi wenye hasira wasiotaka mashindano hayo yafanyike, wengi wamekuwa na hasira juu ya kiasi cha pesa kilichotumika kwa ajili ya maandalizi yake zaidi katika kipindi ambacho nchi inakabiliwa na mtikisiko wa kiuchumi.

Dear readers, after reading the Content please ask for advice and to provide constructive feedback Please Write Relevant Comment with Polite Language.Your comments inspired me to continue blogging. Your opinion much more valuable to me. Thank you.